• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara (MMM) |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Kibaha District Council
Kibaha District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • SP FINAL DRAFT
      • Mazingira na Usafishaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maji
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Maji
    • Afya
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya kisheria
      • Ratiba ya kuonana na mwenyekiti wa halmashauri
    • Kamati za kudumu
      • Fedha Uchumi na Mipango
      • Maadili
      • UKIMWI
      • Huduma za Jamii
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

KUELEKEA KILELE CHA MIAKA 61 YA UHURU MKURUGENZI MTENDAJI PAMOJA NA MENEJIMENTI WAMESHIRIKI KUFANYA USAFI NA KUTOA MSAADA KWA WATOTO YATIMA

Posted on: December 6th, 2022

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Butamo Ndalahwa na watumishi wa Halmashauri hiyo wameshiriki kufanya usafi katika kituo cha afya Mlandizi pamoja na kutoa msaada kwenye vituo vya kulelea watoto.

Shughuli hizo ambazo zimefanyika katika mji mdogo wa Mlandizi ni kati ya vitu vilivyofanywa na Halmashauri hiyo katika maadhimisho ya miaka 61 ya Uhuru ambayo kilele ni Disemba tisa.

Akizungumza baada ya kufanya usafi na kugawa misaada kwa wanawake wajawazito waliokuwa wanapata huduma katika Kituo cha Afya Mlandizi Ndalahwa alimshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa maboresho yanayoendelea kufanyika kwenye sekta ya afya.

Alisema uwepo wa dawa na watoa huduma kwenye kituo hicho imesaidia kwa kipindi cha mwaka mzima kutokuwa na taarifa za vifo kwa Mama na mtoto huku huduma nyingine zikiwa zimeboreka.

"Katika maadhimisho haya tuliamua kufika katika kituo hiki cha afya na kutembelea vituo vinavyolelea watoto Yatima na wanaotoka kwenye mazingira hatarishi ili tuwasikilize vikwazo wanavyokumbana navyo  na Serikali ione namna ya kusaidia kutatua changamoto hizo" alisema Mkurugenzi huyo.

Mganga Mfawidhi wa  kituo Cha afya Mlandizi Dk.Sebastian Misoji alimshukuru Mkurugenzi wa Halmashauri kwa namna ya ufuatiliaji na kushiriki kutatua vikwazo jambo ambalo limesababisha kituo hicho kutoa huduma bora na kutokuwa na vifo vya mama na mtoto kwa mwaka mzima.

Akishukuru baada ya kupokea msaada Mkurugenzi wa kituo cha kulelea watoto cha Upendo Erick Ouma alimshukuru Mkurugenzi kwa kukumbuka kituo hicho na kuwapatia msaada.

Ouma alisema kwasasa kituo hicho kina watoto 19 na wapo ambao wanasoma vyuo, sekondari na shule za msingi.

Vituo vilivyopatiwa misaada hiyo ni pamoja na Vijaliwa vingi, Upendo na Masjid Noor ambavyo vyote vipo ndani ya Mji mdogo wa  Mlandizi vikiwalea watoto wanaotoka katika mazingira hatarishi na yatima.

Matangazo

  • Matokeo ya Darasa La Saba 2022 December 02, 2022
  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Usaili June 28, 2022
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA SENSA KIBAHA DC TAREHE 29-07-2022 July 27, 2022
  • Tangazo la nafasi za kazi May 27, 2022
  • Angalia Vyote

Matukio mapya

  • Kamati ya Siasa ya Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Imefanya Ziara ya Kukagua Miradi ya Maendeleo

    January 27, 2023
  • Halmashauri ya Wilaya ya kibaha Inaendesha Kampeni ya Siku ya Utoaji wa Chanjo ya Polio

    November 23, 2022
  • Shule 10n Bora Kiwilaya Wakabidhiwa Vyeti vya Pongezi na Zawadi

    March 17, 2023
  • Mkuu wa wilaya ya Kibaha Akabidhiwa Ofisi Rasmi .

    January 30, 2023
  • Angalia Vyote

Video

Hotuba ya Rais Magufuli wakati wa Kuzindua bunge
Video Nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TOVUTI YA MKOA WA PWANI
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA AJIRA
  • TOVUTI YA WANANCHI
  • TOVUTI YA BARAZA LA MITIHANI
  • TOVUTI YA WIZARA YA AFYA
  • TOVUTI YA EWURA

Tovuti Zinazoshabihiana

  • TAMISEMI
  • MKOA WA PWANI
  • TANZANIA
  • AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

Free Visitor&Stat Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    KIBAHA DISTRICT COUNCIL

    Anwani ya Posta: P.O BOX 30153

    Simu ya Mezani: +255 23240224

    Simu: +255 0767520048

    Barua pepe: ded.kibaha@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Disclamer
    • Maswali ya mara kwa mara (MMM)
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Kibaha District Council . All rights reserved.