WATUMISHI
Katika kipindi cha miaka kumi iliyopita 2005 mpaka 2015 kumekuwepo na ongezeko la watumishi wa kada mbalimbali kutoka 600 hadi watumishi 1436. Watumishi wapato 602 walishiriki mafunzo, semina warsha na makongamano mbalimbali kwenye vyuo mbalimbali kuwajengea uwezo na kuongezea stadi za kazi kwenye majukumu yao ya kila siku.
Mafunzo ya muda mrefu Shahada ya uzamili, Shahada, Stashahada ya juu Shahada – 38 Mafunzo ya muda mfupi Astashahada 164, na Semina/warsha/kongamamo 400. Pia halmashauri katika kipindi hicho imeajiri watumishi wapatao 836 kwenye Idara mbalimbali. Aidha katika kipindi cha miaka 10 kuanzia mwaka 2005 hadi 2015 watumishi wapatao 672 walithibishwa kazini na kupandishwa cheo.
JEDWARI NA. 2: IDADI YA WATUMISHI
IDARA
|
IDADI YA WATUMISHI |
Idara ya Utawala na Rasilimaliwatu
|
102 |
Idara ya Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
|
4 |
Idara ya Ardhi, Maliasili na Utalii
|
17 |
Idara ya Ujenzi na zimamoto
|
16 |
Idara ya Afya
|
298 |
Idara ya Maendeleo ya Jamii/Ustawi wa Jamii
|
22 |
Idara ya Fedha
|
20 |
Idara ya Maji
|
5 |
Idara ya Mifugo na Uvuvi
|
29 |
Idara ya Kilimo, Ushirika na Umwagiliaji
|
34 |
Idara ya Elimu Sekondari
|
333 |
Idara ya Elimu Msingi
|
514 |
Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
|
3 |
Kitengo cha Sheria
|
1 |
Kitengo cha manunuzi
|
4 |
JUMLA YA WATUMISHI
|
1436 |
Chanzo Idara ya Utumishi 2015
3.0 UTAWALA BORA
Dhana ya Utawala Bora inaendelea kuimarishwa katika nyanja za Demokrasia, Ushirikishwaji wa wananchi, Utawala wa sheria, Uadilifu wa uongozi na watendaji, uwazi na uwajibikaji, ufanisi wa utendaji kazi, uzingatiaji wa jinsia, Taratibu za upangaji mipango shirikishi, stadi za upangaji mipango na matumizi ya takwimu zimezingatiwa ipasavyo na kwa ustadi mkubwa.
Masanduku ya maoni yamewekwa katika sehemu mbalimbali ili wananchi waweze kutoa maoni yao ambapo imesaidia kero mbalimbali za wananchi kuendelea kushughulikiwa. Aidha, taarifa za mapato na matumizi zimekuwa zikitolewa kwa uwazi kwa wananchi.
Mafunzo ya demokrasia yameendelea kutolewa katika wilaya yote na ualikaji wa wananchi kuhudhuria vikao vya Baraza (Full Council) umefanyika kwa ufanisi mkubwa. Halmashauri na Wilaya imekuwa ikifanya vikao vya DCC na Bodi za Zabuni kama ilivyopangwa, na zabuni kutolewa kwa mujibu wa Sheria na Kanuni za manunuzi (The Public Procurement Act, 2004 and The Public Procurement Regulation, 2005).
Vikao vya Halmashauri
Halmashauri ina vikao vifuatavyo;
KIBAHA DISTRICT COUNCIL
Anwani ya Posta: P.O BOX 30153
Simu ya Mezani: +255 23240224
Simu: +255 0767520048
Barua pepe: ded.kibaha@pwani.go.tz
Copyright ©2017 Kibaha District Council . All rights reserved.