• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara (MMM) |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Kibaha District Council
Kibaha District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha

  • Mwanzo
    • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
        • SP FINAL DRAFT
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Afya ,Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasmali Watu
      • Divisheni ya Maendeleo ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Divisheni ya Elimu Sekondari
      • Divisheni ya Miundombinu, Maendeleo ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Usimamizi wa Ununuzi
      • Kitengo cha Usimamizi wa Sheria
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Usafi na Udhibiti wa Taka
      • Kitengo cha Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo, Mifugo na Uvuvi Sehemu ya Mifugo
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Afya ,Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya kisheria
      • Ratiba ya kuonana na mwenyekiti wa halmashauri
    • Kamati za kudumu
      • Fedha Uchumi na Mipango
      • Maadili
      • UKIMWI
      • Huduma za Jamii
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Hatua Kali zichukuliwe kwa Wanaochelewa Kulipa Mikopo

Posted on: June 8th, 2022

MWENYEKITI wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Erasto Makala ameomba Serikali kuandaa sheria kali kwenye utoaji wa mikopo ya asilimia kumi ili kudhibiti wanaokwamisha kwa kutorejesha kwa wakati.

Akizungumza na waandishi wa Habari jana Mjini Mlandizi baada ya kikao cha baraza la Madiwani Makala alisema baadhi ya vikundi vilivyonufaika na mikopo hiyo havijarejesha na hivyo kukwamisha wahitaji wengine kunufaika.

Alisema endapo zitawekwa sheria zitasaidia kuondoa vikwazo vilivyopo sasa ambavyo viasababisha vikundi vinavyohitaji kukwama kupatiwa fedha kuyokana na watu wachache ambao hawajarejesha.

Makala alisema kutokana na hali hiyo Halmashauri kwasasa imejipanga kuchukua hatua za makusudi kwa wadaiwa ambao wanakwamisha malengo ya Halmashauri ya kuwezesha makundi ya Wanawake, Vijana na watu wenye Ulemavu kupata mikopo kwa wakati.

"Mikopo hii ya asilimia kumi sio hisani anayekopa anatakiwa kurejesha ili wengine wanufaike, na Madiwani wasiwatetee hawa wanaodaiwa wasimamie taratibu ili malengo ya Halmashauri ya kuyawezesha makundi yanayolengwa yafikiwe" alisisitiza.

Mwenyekiti huyo alisema wameshatoa maagizo kwa watendaji wa Kata kuhakikisha wanachukua hatua kwa vikundi vilivyokopa virejeshe fedha hizo lakini pia wametoa miongozo kwa Maofisa Maendeleo ya jamii kushughulikia suala hilo kwani linasababisha kuwepo kwa hoja kwa wakaguzi wa hesabu za ndani na nje.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Ruth Mwelo alisema vikundi vinavyopata mikopo vinatakiwa kupata elimu kuhakikisha wanarejesha fedha za mikopo kwa kuweka benki na si kuwapatia watumishi wawarejeshee.

Alisema watumishi wanaosimamia urejeshaji wa mikopo hususani wa Maendeleo ya jamii ngazi ya kata wanatakiwa wahakikishe wanakuwa waadilifu, waaminifu kwa mujibu wa sheria kwa kufanya kazi kwa kufuta taratibu kwa kutopokea fedha za vikundi za marejesho kutoka kwenye vikundi.

"Hairuhusiwi mtu yeyote hata kama ni msimamizi wa mikopo kupewa fedha mkononi kwasababu baadhi yao wamekosa uaminifu kwa kurejesha fedha hizo benki na hivyo kufanya Halmashauri kupata hasara.

Na hii ya kuwapatia wataalamu imesababisha baadhi ya vikundi kuonekana bado vinadaiwa wakati fedha wamewakabidhi wataalamu jambo ambalo ni kinyume na taratibu" alisema

Ruth alisema wakati mwingine hali hiyo inasababisha Halmashauri kupata hasara pale fedha hizo zikiwa hazirejeshwi na wengine kukosa fursa ya kukopa.

Mwenyekiti wa Kamati ya huduma za Jamii Josephine Gunda alisema wadaiwa wa mikopo ya Halmashauri wanatakiwa kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria ili vikundi vingine vinavyohitaji kukopa vinufaike kwa wakati.

Gunda alisema ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo intakiwa kuwachukulia hatua ili kukomesha tabia hiyo ambayo inawanyima wengine kunufaika.

Matangazo

  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI WA BVR HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBAHA January 23, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI September 23, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI September 23, 2024
  • MABADILIKO YA TAREHE YA USAILI September 24, 2024
  • Angalia Vyote

Matukio mapya

  • KAIMU KATIBU TAWALA WILAYA YA KIBAHA ATOA WITO KWA WENYEVITI WA MJI MDOGO MLANDIZI KUZINGATIA UADILIFU

    February 11, 2025
  • MAKAMU WA RAIS AZINDUA MBIO ZA MWENGE WA UHURU, ATOA WITO DHIDI YA UBADHILIFU

    April 02, 2025
  • ELIMU YA LISHE JUU YA USINDIKAJI WA BIDHAA ZA VYAKULA YATOLEWA KIBAHA DC.

    March 23, 2025
  • Mwenyekiti wa Halmashauri Amshukuru Rais Samia kwa Fedha za Miradi

    February 05, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Hotuba ya Rais Magufuli wakati wa Kuzindua bunge
Video Nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TOVUTI YA MKOA WA PWANI
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA AJIRA
  • TOVUTI YA WANANCHI
  • TOVUTI YA BARAZA LA MITIHANI
  • TOVUTI YA WIZARA YA AFYA
  • TOVUTI YA EWURA

Tovuti Zinazoshabihiana

  • TAMISEMI
  • MKOA WA PWANI
  • TANZANIA
  • AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

Free Visitor&Stat Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    KIBAHA DISTRICT COUNCIL

    Anwani ya Posta: P.O BOX 30153

    Simu ya Mezani: +255 23240224

    Simu: +255 0767520048

    Barua pepe: ded.kibaha@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Disclamer
    • Maswali ya mara kwa mara (MMM)
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Kibaha District Council . All rights reserved.