• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara (MMM) |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Kibaha District Council
Kibaha District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • SP FINAL DRAFT
      • Mazingira na Usafishaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maji
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Maji
    • Afya
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya kisheria
      • Ratiba ya kuonana na mwenyekiti wa halmashauri
    • Kamati za kudumu
      • Fedha Uchumi na Mipango
      • Maadili
      • UKIMWI
      • Huduma za Jamii
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Hatua Kali zichukuliwe kwa Wanaochelewa Kulipa Mikopo

Posted on: June 8th, 2022

MWENYEKITI wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Erasto Makala ameomba Serikali kuandaa sheria kali kwenye utoaji wa mikopo ya asilimia kumi ili kudhibiti wanaokwamisha kwa kutorejesha kwa wakati.

Akizungumza na waandishi wa Habari jana Mjini Mlandizi baada ya kikao cha baraza la Madiwani Makala alisema baadhi ya vikundi vilivyonufaika na mikopo hiyo havijarejesha na hivyo kukwamisha wahitaji wengine kunufaika.

Alisema endapo zitawekwa sheria zitasaidia kuondoa vikwazo vilivyopo sasa ambavyo viasababisha vikundi vinavyohitaji kukwama kupatiwa fedha kuyokana na watu wachache ambao hawajarejesha.

Makala alisema kutokana na hali hiyo Halmashauri kwasasa imejipanga kuchukua hatua za makusudi kwa wadaiwa ambao wanakwamisha malengo ya Halmashauri ya kuwezesha makundi ya Wanawake, Vijana na watu wenye Ulemavu kupata mikopo kwa wakati.

"Mikopo hii ya asilimia kumi sio hisani anayekopa anatakiwa kurejesha ili wengine wanufaike, na Madiwani wasiwatetee hawa wanaodaiwa wasimamie taratibu ili malengo ya Halmashauri ya kuyawezesha makundi yanayolengwa yafikiwe" alisisitiza.

Mwenyekiti huyo alisema wameshatoa maagizo kwa watendaji wa Kata kuhakikisha wanachukua hatua kwa vikundi vilivyokopa virejeshe fedha hizo lakini pia wametoa miongozo kwa Maofisa Maendeleo ya jamii kushughulikia suala hilo kwani linasababisha kuwepo kwa hoja kwa wakaguzi wa hesabu za ndani na nje.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Ruth Mwelo alisema vikundi vinavyopata mikopo vinatakiwa kupata elimu kuhakikisha wanarejesha fedha za mikopo kwa kuweka benki na si kuwapatia watumishi wawarejeshee.

Alisema watumishi wanaosimamia urejeshaji wa mikopo hususani wa Maendeleo ya jamii ngazi ya kata wanatakiwa wahakikishe wanakuwa waadilifu, waaminifu kwa mujibu wa sheria kwa kufanya kazi kwa kufuta taratibu kwa kutopokea fedha za vikundi za marejesho kutoka kwenye vikundi.

"Hairuhusiwi mtu yeyote hata kama ni msimamizi wa mikopo kupewa fedha mkononi kwasababu baadhi yao wamekosa uaminifu kwa kurejesha fedha hizo benki na hivyo kufanya Halmashauri kupata hasara.

Na hii ya kuwapatia wataalamu imesababisha baadhi ya vikundi kuonekana bado vinadaiwa wakati fedha wamewakabidhi wataalamu jambo ambalo ni kinyume na taratibu" alisema

Ruth alisema wakati mwingine hali hiyo inasababisha Halmashauri kupata hasara pale fedha hizo zikiwa hazirejeshwi na wengine kukosa fursa ya kukopa.

Mwenyekiti wa Kamati ya huduma za Jamii Josephine Gunda alisema wadaiwa wa mikopo ya Halmashauri wanatakiwa kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria ili vikundi vingine vinavyohitaji kukopa vinufaike kwa wakati.

Gunda alisema ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo intakiwa kuwachukulia hatua ili kukomesha tabia hiyo ambayo inawanyima wengine kunufaika.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Usaili June 28, 2022
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA SENSA KIBAHA DC TAREHE 29-07-2022 July 27, 2022
  • Tangazo la nafasi za kazi May 27, 2022
  • TANGAZO KWA WATUMISHI AJIRA MPYA July 04, 2022
  • Angalia Vyote

Matukio mapya

  • Kamati ya Fedha Mipango na Uongozi Imefanya ziara ya Kukagua miradi

    July 25, 2022
  • Wakulima wa Korosho Wameomba Serikali Iwasidie Kudhibiti Wizi wa Korosho Mashambani

    July 08, 2022
  • Halmashauri ya Wilaya ya kibaha Imefanya Maadhimisho ya siku ya afya ya Kijiji

    July 05, 2022
  • Waliosababisha Hasara Katika Hoja za Ukaguzi wa Mahesabu Wachukuliwe Hatua -Rc Kunenge

    June 16, 2022
  • Angalia Vyote

Video

Hotuba ya Rais Magufuli wakati wa Kuzindua bunge
Video Nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TOVUTI YA MKOA WA PWANI
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA AJIRA
  • TOVUTI YA WANANCHI
  • TOVUTI YA BARAZA LA MITIHANI
  • TOVUTI YA WIZARA YA AFYA
  • TOVUTI YA EWURA

Tovuti Zinazoshabihiana

  • TAMISEMI
  • MKOA WA PWANI
  • TANZANIA
  • AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

Free Visitor&Stat Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    KIBAHA DISTRICT COUNCIL

    Anwani ya Posta: P.O BOX 30153

    Simu ya Mezani: +255 23240224

    Simu: +255 0767520048

    Barua pepe: ded.kibaha@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Disclamer
    • Maswali ya mara kwa mara (MMM)
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Kibaha District Council . All rights reserved.