• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara (MMM) |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Kibaha District Council
Kibaha District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • SP FINAL DRAFT
      • Mazingira na Usafishaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maji
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Maji
    • Afya
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya kisheria
      • Ratiba ya kuonana na mwenyekiti wa halmashauri
    • Kamati za kudumu
      • Fedha Uchumi na Mipango
      • Maadili
      • UKIMWI
      • Huduma za Jamii
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha imekabidhi Madarasa 30 kwa Mkuu wa Willaya ya Kibaha

Posted on: January 14th, 2022

Kukamilika kwa ujenzi wa vyumba 30 vya madarasa kwa shule za msingi na Sekondari Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani kutawezesha uwepo wa ongezeko la wanafunzi kutoka 7,275 hadi kufikia 8690  hali inayoelezwa kuwa ni njia moja wapo ya kuinua kiwango cha Elimu kwa jamii.

Kabla ya ujenzi huo Halamashauri hiyo imekuwa na changamoto ya upungufu wa vyumba vya madarasa 7 hali ambayo imekuwa ikisababisha wanafunzi kusoma wakiwa wamelundikana kwa chumba kimoja zaidi ya 50 hivyo kushindwa kusoma kwa nafasi.

Kwa mujibu wa taarifa ya Afisa Elimu Halmashauri hiyo aliyoisoma kwa Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Sara Msafiri jana alisema kuwa ujenzi wa madarasa hayo umetokana na pesa za uvico na kwamba mpaka sasa wameshakamilisha ujenzi kwa asilimia 100.


Alisema kuwa Halmashauri hiyo ilipokea sh. m. 600 kwaajili ya ujenzi wa vyumba 30 vya madarasa ambapo kati ya hivyo 20 vya shule ya sekondari na 10 ni upande wa shule za msingi.

Alisema kuwa katika ujenzi huo pia wamefanikiwa kujenga shule mpya ambazo zitawezesha kupokea wanafunzi wa sekondari wa kidato cha kwanza na wale wa vidato vingine ambao awali walikuwa walikuwa wanalazimika kutembea umbali wa km 10 kwa siku kufuata masomo kutokana umbali wa makazi na maeneo ya shule.

"Mpaka sasa tumeshakamilisha hatua zote na tuna uhakika kuwa jumatatu ya january 17 wanafunzi wote wataanza masomo na hatutakuwa na awamu mbili za kuwapangia shule wanafunzi wote waliofaulu"alisema.

Mbunge wa Jimbo la Kibaha Vijijini Michael Mwakamo aliwataka walimu na wanafunzi watakaoyatumia madawati pamoja na madarasa hayo kuyatunza ili yatumike kwa vizazi vilivyopo na vile vijavyo.

"Akizungumza baada ya kupokea vyumba hivyo vya madarasa Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Sara Msafiri alisema kuwa wanafunzi wa shule za sekondari na msingi Wilayani huko watakaobainika kuvunja madawati kwa makusudi wazazi wao wataajibika kulipa ili kulipa mafundi watakaotengeneza.

Alisema kuwa kutokana n juhudi zilizofanywa naSerikali kukopa pesa na kughalimia ujenzi huo halipaswi kuweka mchezo na kuwafumbia macho watu wachache watakaoonekana kurudisha nyuma jitihada hizo.



Matangazo

  • Tangazo Maalum kwa waajiriwa Wapya kada za Afya na Elimu July 05, 2021
  • Tangazo la Uuzaji wa Viwanja Lupunga June 22, 2021
  • WANAHITAJIKA MAFUNDI WA KAZI ZA UJENZI KWA MATUMIZI YA NJIA YA "FORCE ACCOUNT" January 05, 2021
  • Wafanyabiashara ya mazao ya chakula September 14, 2018
  • Angalia Vyote

Matukio mapya

  • MAKALA MAALUM YA SIKU 365 ZA MHE. SAMIA SULUHU HASSAN RAIS WA JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

    March 19, 2022
  • WAFUGAJI WASIMAMIWE SOKO LA BIDHAA ZA MIFUGO ILI KUWAONGEZEA KIPATO

    May 13, 2022
  • Viongozi Watakiwa Kusimamia Miradi ya Maendeleo kwa Weledi

    May 08, 2022
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha imekabidhi Madarasa 30 kwa Mkuu wa Willaya ya Kibaha

    January 14, 2022
  • Angalia Vyote

Video

Hotuba ya Rais Magufuli wakati wa Kuzindua bunge
Video Nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TOVUTI YA MKOA WA PWANI
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA AJIRA
  • TOVUTI YA WANANCHI
  • TOVUTI YA BARAZA LA MITIHANI
  • TOVUTI YA WIZARA YA AFYA
  • TOVUTI YA EWURA

Tovuti Zinazoshabihiana

  • TAMISEMI
  • MKOA WA PWANI
  • TANZANIA
  • AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

Free Visitor&Stat Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    KIBAHA DISTRICT COUNCIL

    Anwani ya Posta: P.O BOX 30153

    Simu ya Mezani: +255 23240224

    Simu: +255 0767520048

    Barua pepe: ded.kibaha@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Disclamer
    • Maswali ya mara kwa mara (MMM)
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Kibaha District Council . All rights reserved.