• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara (MMM) |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Kibaha District Council
Kibaha District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • SP FINAL DRAFT
      • Mazingira na Usafishaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maji
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Ufugaji wa Nyuki
      • Uchaguzi
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Maji
    • Afya
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya kisheria
      • Ratiba ya kuonana na mwenyekiti wa halmashauri
    • Kamati za kudumu
      • Fedha Uchumi na Mipango
      • Maadili
      • UKIMWI
      • Huduma za Jamii
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Kandege Aipigia Salute ya Kampeni ya Elimisha Kibaha

Posted on: June 24th, 2020

Naibu Waziri wa TAMISEMI Mhe. Josephat Kandege amezindua madarasa 32 na ofisi nne za walimu katika shule za sekondari,yaliyojengwa kupitia kampeni ya ELIMISHA KIBAHA,mkoani Pwani ambayo yatapunguza changamoto iliyokuwepo awali ya mlundikano wa wanafunzi madarasani na yatatumiwa na wanafunzi takriban 900.

Katika hafla hiyo ya kukabidhi madarasa hayo,amewaasa wazazi na walezi kuwapa elimu watoto wao na kuhakikisha wanafuatilia maendeleo ya taaluma zao ili baadae watumie fursa ya viwanda vinavyojengwa kwa wingi mkoani humo .

Alisema ELIMISHA KIBAHA ni kuunga mkono jitihada za Rais Magufuli za kuhakikisha elimu inatolewa bure kwa kila mwanafunzi wa darasa la awali hadi kidato cha nne.

“Haya ni maelekezo ya ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2015,ambayo nina ujasiri wa kusema ninyi Kibaha, mmetekeleza,na nawaagiza wakuu wa wilaya wengine waige mfano wako mkuu wa wilaya ya Kibaha ambae umebuni kampeni hii na kuzaa matunda”alisema Kandege.

Alieleza, hii ni hatua kubwa ,kwani kama mkuu huyo wa wilaya angekaa kusubiri ruzuku ya serikali kuu ama mapato ya halmashauri ndiyo yajenge azma hii isingetimia kwa mwaka mmoja huu.

Kandege alifafanua ,kiuhalisia haiwezekani kuwa na Taifa lililoelimika kama hakuna mazingira bora ya sekta ya elimu ,hali itakayofanya watanzania wawe na ujuzi wa kutosha katika matumizi ya rasilimali zilizopo na fikra chanya za maendeleo. Hivyo,ubunifu uliofanyika umelenga katika kufikia malengo ya dira ya maendeleo ya Taifa ya mwaka 2025.

‘”Mkoa wa Pwani umejikita katika uwekeaji wa viwanda ambapo kuna viwanda 47 ambavyo ni vikubwa,vya kati na vidogo vinavyofanyakazi,hii ni fursa kwa wanafunzi kuchangamkia ,kwani bila vijana wetu kuwa na elimu nafasi za kazi za kitaalamu kwenye viwanda hivyo vitachukuliwa na vijana wa mikoa mingine na nje ya nchi.”alisema Kandege.

Nae Mkuu wa wilaya ya Kibaha, Mhe.Assumpter Mshama amesema chimbuko la kampeni ya elimisha Kibaha limetokana na upungufu wa madarasa uliojitokeza mwaka 2019 kutokana na kuongezeka kwa ufaulu mwaka 2018 hali iliyosababisha baadhi ya shule wanafunzi waingie kwa awamu mbili.

“Kufuatia hali hii nilishirikiana na wadau wa maendendeleo ili kuondoa upungufu wa madarasa uliopo kwa halmashauri ya wilaya madarasa 34 na halmashauri ya Mji 

Matangazo

  • Wadaiwa wa Viwanja kibaha June 15, 2020
  • WANAHITAJIKA MAFUNDI WA KAZI ZA UJENZI KWA MATUMIZI YA NJIA YA "FORCE ACCOUNT" January 05, 2021
  • Matokeo ya Kidato cha Sita Shule za Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha July 11, 2019
  • Kuhamia Mji Mdogo wa Mlandizi October 31, 2019
  • Angalia Vyote

Matukio mapya

  • Halmashauri ya wilaya ya kibaha Imeendesha Mafunzo ya Kuwajengea Uwezo Wahe.Madiwani.

    December 15, 2020
  • Mwakamo Aridhishwa na Matumizi ya Fedha

    December 03, 2020
  • Kibaha Dc Wakabidhi Madawati 127 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kibaha kutekeleza Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Pwani Kuhusu Utengenezaji wa Madawati Katika Shule za Sekondari

    September 11, 2020
  • Mkuu wa Wilaya Awataka Watoa Huduma Watekeleze Wajibu Wao kwa Weledi

    August 04, 2020
  • Angalia Vyote

Video

Hotuba ya Rais Magufuli wakati wa Kuzindua bunge
Video Nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • TOVUTI YA MKOA WA PWANI
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA AJIRA
  • TOVUTI YA WANANCHI
  • TOVUTI YA BARAZA LA MITIHANI
  • TOVUTI YA WIZARA YA AFYA
  • TOVUTI YA EWURA

Tovuti Zinazoshabihiana

  • TAMISEMI
  • MKOA WA PWANI
  • TANZANIA
  • AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

Free Visitor&Stat Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    KIBAHA DISTRICT COUNCIL

    Anwani ya Posta: P.O BOX 30153

    Simu ya Mezani: +255 23240224

    Simu: +255 0767520048

    Barua pepe: ded.kibaha@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Disclamer
    • Maswali ya mara kwa mara (MMM)
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Kibaha District Council . All rights reserved.