Kabla ya Uhuru katika eneo letu la Mlandizi Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha tulikuwa tunatembea km 36 kwenda shule tofauti na ilivyo sasa lakini pia usafiri wa kwenda Dar es Salaam ilikuwa lazima tupande treni" alisema Mohamed Pongwe.
Mohamed Pongwe ni kati ya wazee wakongwe wanaoishi katika mji mdogo wa Mlandizi ambaye alihamia hapo tangu mwaka 1956.
Akizungumza jana mjini Mlandizi kuhusiana na mabadiliko ya kimaendeleo kabla ya Uhuru na hali ilivyo sasa ambapo alisema pamoja na kutokamilika kwa mahitaji kama inavyotakiwa lakini yapo ambayo wanaweza kuyaelezea.
Pongwe alieleza kuwa waliobahatika kusoma wengi wao walikuwa wakitembea umbali wa km 36 kwenda kupata huduma ya elimu katika shule ya msingi iliyokuwa katika eneo la Mzenga.
Pongwe anasema kwa sasa shule zimetapakaa watoto hawatembei umbali mrefu kupata huduma tena anasema elimu inatolewa bure watoto wanatakiwa kuvaa unifomu madawati wanayakuta shuleni bila gharama.
"Hata ukitaka kwenda Mkoa wa Dar es Salam tulikuwa tunatumia treni unatembea kutoka Mlandizi hadi Ruvu stesheni kusubiri treni hakukuwa na barabara zaidi ya njia ya kusafirisha watumwa iliyokuwa inaenda Bagamoyo" aliongeza.
“ Huduma za kijamiii zimeimarika kwani hospitali zimejengwa kila kona mfano kituo cha afya Mlandizi huduma zinazotolewa utadhani ni hospitali kubwa kwani huduma zote zinapatikana tena tumeletewa hospitali ya wilaya tunaishukuru sana serikali yetu kwa kweli mabadiliko ni makubwa sana “ Alisema Pongwe
Pia Pongwe Aliiomba Serikali kuwatengenezea mazingira ya kilimo cha umwagiliaji ambacho wanakuona kitakuwa na tija kwao.
Omari Hassani mkazi wa Mlandizi ambaye alisema alihamia katika Halmashauri hiyo tangu mwaka 1938 alisema yapo mabadiliko makubwa yamefanyika tangu uhuru .
Hassani alisema Serikali imeleta mabadiliko hususan kwenye huduma za afya ambapo wazee wana dirisha maalumu la kupata huduma jambo ambalo halikuwepo awali.
Pia Hospitali zimeboreshwa madawa yanapatikana aliishukuru Serikali kwa kuwaletea hospitali ya wilaya kwani anaamini huduma zote muhimu zitapatikana
“Tangu uhuru hatukuwa na Hospitali ya Wilaya tulikuwa tunatibiwa kwenye Zahanati na Vituo vya afya huduma nyingi tulikuwa tunaambiwa tuzifuate Tumbi lakini saivi serikali yetu imetuletea hospitali kwa kweli sisi wazee tunafurahi sana tunaishukuru serikali yetu kwa kutujali sisi wananchi wake” alisema Hassan
Wazee wengine katika eneo la Mlandizi walimshukuru Mhe. Dk.Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa namna alivyoboresha huduma za kijamii hali inayoleta hamasa kwa wanafunzi kusoma kwa bidii kutokana na mazingira mazuri ya kujisomea yaliyopo.
KIBAHA DISTRICT COUNCIL
Anwani ya Posta: P.O BOX 30153
Simu ya Mezani: +255 23240224
Simu: +255 0767520048
Barua pepe: ded.kibaha@pwani.go.tz
Copyright ©2017 Kibaha District Council . All rights reserved.