WANANCHI WAIPONGEZA SERIKALI KWA KUWASOGEZEA HUDUMA ZA AFYA KARIBU NA MAKAZI.
Wananchi wa Kata za Boko Mnemela na Soga wameipongeza Serikali kwa kuwaunga mkono juhudi zao za kusogeza huduma za afya karibu na makazi yao.
Hayo yamesemwa wakati ya ziara ya kamati ya Fedha na mipango ya kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa nguvu za wananchi kwa madhumuni ya kuwaongezea nguvu katika kumalizia miradi hiyo.
Kamati hiyo ilitembelea ujenzi wa Zahanati ya Mpiji,Kipangege , Msufini na Ruvu Station.
Akiwasilisha taarifa ya ujenzi wa Zahanati ya kijiji cha Mpiji Afisa mtendaji wa Kijiji hicho alisema walianza mchakato wa wa ujenzi wa zahanati mwaka 2019 baada ya wajumbe wa serikali ya Kijiji kuibua mradi huo wa Zahanati ambao hadi kukamilika utagharimu kiasi cha milioni mia moja.
Wananchi wa kijiji cha mpiji wamefanikiwa kujenga zahanati hiyo hadi kufikia hatua ya boma kwa shilingi milioni thelathini na tatu . kwa kuunga juhudi zao hizo serikali kuu imetoa shilingi milioni hamsini kwa ajili ya kumalizia ujenzi huo.
Akiongea wakati wa ziara hiyo diwani ya kata ya Bokomnemela MhePaul Maguhwa amesema anaishukuru sana serikali kwa kuona juhudi za wananchi na kuwaunga mkono kwani wananchi watapata moyo wa kuendelea kuchangia maendeleo kwenye vijiji vyao.
Aidha wanachi wa kijiji cha kipangeje wameishukuru Serikali kwa kuunga mkono jitihadi zao za ujenzi wa zahanati ya kijiji kwani walikuwa wanapatashida sana za kufata huduma za afya katika kijiji cha Soga.
”wananchi wa Kipangege tunapata shida sana ya Zahanati mimi nimemwambia mke wangu asizae kutokana na umbali uliopo kutoka hapa hadi zahanati ya Soga” alisema Omary Hamis mjumbe wa kamati ya uchangishaji wa ujenzi wa Zahanati ya Kipangeje
Wanannchi wa wa vijiji hivyo wamekuwa wakitembea umbali mrefu kufata huduma za afya kwenye zahanati za vijiji jirani.
Mwenyekiti wa Halmshauri ya Wilaya ya Kibaha Mhe. Erasto Mkala amewapongeza wananchi wa vijiji hivyo kwa kuibua miradi na kuisimamia ipasavyo kwani ujenzi wa Zahanati hizo umetekelezwa kwa ubora unaotakiwa na kuwataka kuendelea kusimamia miradi hiyo kwa ukaribu .
KIBAHA DISTRICT COUNCIL
Anwani ya Posta: P.O BOX 30153
Simu ya Mezani: +255 23240224
Simu: +255 0767520048
Barua pepe: ded.kibaha@pwani.go.tz
Copyright ©2017 Kibaha District Council . All rights reserved.