Aliyekuwa mkuu wa wilaya ya kibaha Sara Msafiri amemkabidhi rasmi ofisi mkuu mpya wa Wilaya ya Kibaha Mhe.Nickson John makabidhiano hayo yamefanyika katika Halmashauri ya mji Kibaha na kushuhudiwa na kamati ya ulinzi na usalama, wenyeviti wa halmashauri zote mbili pamoja na watendaji kutoka taasis mbali mbali za serikali.
Akiongea kwenye makabidhiano hayo Sara amezikushuru halmashauri pamoja na tasisi za serikali viongozi wa dini kwa ushirikiano waliompa kwa kipindi chote alichofanya kazi kibaha.
“niwashukuru Wakurugenzi wangu na kamati ya ulinzi na usalama mmenipa ushirikano hakuna mahali tumewahi kushindwa kila lilipotokea jambo tulishirikiana kwa karibu ,naamini teamwork pays mkifanya kazi kwa ushirikiano lazima mtashinda niwaombe ushirikiano mlionipa muonyeshe kwa Dc mpya ili tuzidi kumsaidia Mhe. Rais”
Sara amesema amejifunza vitu vingi sana alipokuwa mkuu wa wilaya ikiwemo utawala hivyo atatumia ujuzi huo kuendelea mbele.
Mkuu wa wilaya ya Kibaha Nickson amesema anaamini katika teamwork anaamini watu wakifanya kazi kwa ushirikiano kazi zitaenda vizuri hivyo kuwataka watumishi kufanya kazi kwa kushirikiana ili kuleta maendeleo katika wilaya ya Kibaha.
Nickson ameziomba taasis zote na Halmashauri kushirikiana nae kwenye kazi ili kuweza kutengeneza ndoto ya pamoja ya kuleta maendeleo kwa wananchi wa Kibaha.
Akiongea kwenye makabidhiano hayo Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kibaha Mhe. Erasto Makala amempongeza Sara kwa juhudi alizoonyesha alipokuwa Mkuu wa wilaya kwani miradi mingi imejengwa Kibaha chini ya uongozi wake.
Makala amempongeza Nicksoni kwa kuendelea kuaminiwa na Mhe. Rais na kumuahidi kumpa ushirikiano wa kutosha .
“Nickson sio mgeni kwenye ukuu wa Wilaya najua amefanya vizuri Kisarawe naomba niamini kwenye ndoto ulizosema , kibaha tunaamini kwenye teamwork nikuhakikishie sisi wenyeviti tutakupa ushirikiano wa kustosha” alisema Makala.
Mwenyekiti wa Halmshauri ya Kibaha mji Mhe.Ndomba amemshukuru Sara kwa utendaji mzuri na kusema ameacha alama kwani alikuwa anaweza kuingia sehemu ambayo watu wengine hawawezi kuingia .
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya kibaha Butamo Ndalahwa amesema Sara ameacha alama kwani chini ya uongozi wake halamshauri hiyo iliweza kushika namba moja katika ukuasanyaji mapato.
Pia aliweza kusimamia uazishwaji wa kongani za viwanda ya Disunyara na kwala . Butamo amemuhakikishia mkuu wa wilaya kuwa yeye na Cmt yake watampa ushirikiano wa kutosha .
KIBAHA DISTRICT COUNCIL
Anwani ya Posta: P.O BOX 30153
Simu ya Mezani: +255 23240224
Simu: +255 0767520048
Barua pepe: ded.kibaha@pwani.go.tz
Copyright ©2017 Kibaha District Council . All rights reserved.