Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Dkt.Seleman Jafo amezindua kampeni ya Mazingira na matumizi ya Nishati mbadala pamoja na mashindano ya upandaji miti .
Uzinduzi huo umefanyika Leo tarehe 19.04.2023 katika shule ya Sekondari ya wasichana Ruvu ,Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani.
Akiongea wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo amesisitiza matumizi ya Nishati mbadala katika Taasisi za umma na binafsi zenye watu zaidi ya 100 ,ili kuokoa gharama kubwa zinazotumika katika manunuzi ya mkaa na kuni.
Mhe.Jafo amehimiza wananchi kuungana katika Utunzaji na kulinda Mazingira ili kuepukana na mabadiliko ya tabia nchi ambayo yanaathiri Mazingira na Uchumi.
Aidha Jafo Alieleza lengo kubwa ni kusonga mbele katika kudhibiti uharibifu wa Mazingira,ukataji miti ambapo Serikali ilishatoa tamko Taasisi hizo kujikita na matumizi ya Nishati mbadala na maelekezo hayo hayakugusa mwananchi mmoja mmoja licha ya kwamba wananchi wanatakiwa kutunza Mazingira na kuacha kukata miti ovyo.
"Niwapongeze Taifa gas kwa kuwafungia mtungi wa gesi wa milioni sita katika shule ya Sekondari ya wasichana Ruvu kwa ajili ya matumizi ya jiko la shule hii ,na Leo huu ni ushuhuda tosha kuona kwamba mambo haya yanawezekana."
Kama Sekondari zote zikiweka Utaratibu na Taifa gas kuweza kufungiwa gas shule zote za bweni ,zitatumia Nishati mbadala na kuweza kuokoa kiasi kikubwa cha fedha,"anafafanua Jafo.
Akitoa salamu za Mkoa , Mwakilishi wa mkuu wa Mkoa wa Pwani,mkuu wa wilaya ya Kibaha Mhe. Nickson Simon alisema ,mkoa huo una changamoto kubwa ya kimazingira hivyo wameamua kujipambanua katika upande wa mazingira ili kupambana na hali hiyo.
Alieleza, mkoa umeshapanda miti milioni Tisa sawa na asilimia 82 ,lengo likiwa kupanda miti zaidi ya milioni 13.
Vilevile ,wamejipanga kuongeza usimamizi wa mazingira, upandaji miti, teknolojia mbadala na uchumi.
KIBAHA DISTRICT COUNCIL
Anwani ya Posta: P.O BOX 30153
Simu ya Mezani: +255 23240224
Simu: +255 0767520048
Barua pepe: ded.kibaha@pwani.go.tz
Copyright ©2017 Kibaha District Council . All rights reserved.