KIBAHA DC WAKABIDHI MADAWATI 127 KWA MKUU WA WILAYA YA KIBAHA KUTEKELEZA AGIZO LA MKUU WA MKOA WA PWANI KUHUSU UTENGENEZAJI WA MADAWATI KATIKA SHULE ZA SEKONDARI.
Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Mhe. Martin Mtemo amepokea madawati 127 kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha ikiwa ni juhudi za kutekeleza agizo la Mkuu wa Mkoa wa Pwani la kutengeneza madawati katika shule za secondari ifikapo mwisho wa mwezi wa tisa.
Makabidhiano hayo yamefanyika leo katika shule ya sekondari Kilangalanga,akiongea wakati wa makabidhiano hayo Mtemo ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha kwa kutekeleza agizo hilo kwa wakati na mikakati mizuri waliyojiwekea kumaliza tatizo hilo. amewataka wahakikishe upungufu wa madawati kwa shule za sekondari unamalizika ifikapo mwisho wa mwezi wa tisa.
Pamoja na pongezi hizo Mkuu wa Wilaya amewataka watendaji kuhakikisha ubora wa madawati hayo”nasisitiza wakati mnatekeleza agizo la kutengeneza madawati mzingatie ubora”alisisitiza Mtemo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Bi.Butamo Ndalahwa amesema jumla ya madawati 149 yametengenezwa na kukamilika, madawati 127 yamekarabatiwa na kukamilika na madawati 160 yameanza kutengenezwa na madawati 251 ukarabati wake unaendelea Na hivyo kufanya upungufu wa madawati kufikia 372kutoka 1059.
Aidha Bi. Butamo amesema jitihada zaidi zinaendelea ikiwa ni pamoja na kuwashirikisha wadau mbalimbali wa maendeleo wa maendeleo ndani nan je ya Mkoa.
KIBAHA DISTRICT COUNCIL
Anwani ya Posta: P.O BOX 30153
Simu ya Mezani: +255 23240224
Simu: +255 0767520048
Barua pepe: ded.kibaha@pwani.go.tz
Copyright ©2017 Kibaha District Council . All rights reserved.